MTUME NYAGA HR

AGALIA EMMANUEL TV LIVE [WATCH EMMANUEL TV LIVE]

Jumanne, 29 Aprili 2014

SIKU YA NNE: MWINJILISTI JAILOS MALODA NA MTUME PETER NYAGA KATIKA KAULI MBIU YAO YA "MOROGORO YOTE KWA YESU" YALETA MATUNDA SIKU YA JUMATATU

Watu wamemiminika kama mvua katika mkutano unaoendelea katika viwanja vya K/Ndege mkoani Morogoro siku ya Jumatatu. Watu wamefika pale mapema sana kupokea ujumbe wa Yesu Kristo kwa kupitia watumishi hawa wawili yaani mwinjilisti Jailos Maloda wa Morogoro na Mtume Peter Nyaga wa kanisa la RGC Tabata Dar es Salaam. Idadi ya watu waliokoka kwa makadilio inasemekana ni kama watu 200 waliofika mbele ya jukwaa na kuungama dhambi zao mbele ya maelfu ya watu na kukiri kuwa walikuwa wakosaji na sasa wameyakabidhi maisha yao kwa Bwana Yesu Kristo.

Katika kutano huu kulikiwa na waimbaji mbalimbali kama vile Masanja Mkandamizaji, Mess Jacob Chengula, Joshua Makondeko na wengine weni ambao kwa kupitia karama zao za uimbaji waliweza kugeuza mioyo ya watu na wakampokea Bwana Yesu Kristo siku hii ya Jumatatu










 Mtume Peter Nyaga akisalimiana na mwimbaji wa nyimbo za injili Joshua Makondeko




 Mtume Peter Nyaga akisalimiana na Masanja Mkandamizaji


 Mtume Peter Nyaga (kushoto) akiwa na Mess Jacob Chengula
 Mess Jacob Chengula akijiweka sawa kwa kazi ya Mungu kwa njia ya uimbaji

 Msanja Mkandamizaji akiwaleta watu wa Mungu kwa Bwana Yesu kwa njia ya uimbaji


"MOROGORO YOTE KWA YESU" YAZIDI KULETA MATUNDA MAKUBWA KWA KUPITIA MTUME PETER NYAGA NA MWINJILIST JAILOS MALODA MKOANI MORORGORO

Watu zaidi 200 wachia maisha yao kwa Yesu Kristo baada ya kupata ujumbe wa Mungu kwa kupitia watumishi wake wanaofanya kazi ya Mungu kama punda katika mkoa wa Mororgoro. Kama kauli mbiu inavyosema, Morogoro Yote kwa Yesu, watumishi hawa kwa msaada wa Mungu wamejipanga watu wote wa mkoa wa Mororgoro kuokoka,



MTUME PETER NYAGA NA MWINJILSTI JAILO MALODA WAFANAYA MAKUU KATIKA MKUTANO WA MOROGORO YOTE KWA YESU SIKU YA JUMAPILI

"Morogoro Yote kwa Yesu" huo ndio usemi unayotamba sasa mkoani Morogoro kwa sasa, watumishi wa Mungu wameandaa mkutano huu wa kumtangaza Yesu Kristo na kuwafungua watu waliofungwa na mateso mbalimbali. Siku ya Jumapili watu walimimika katika eneo la tukio kushuhudia jinsi gani Mungu anafanya makuu kwa kupitia watumishi wake waliopo hapa dunia. Watu wenye mapepo walionekana kugalagala chini wakihangaika na kulia kwa maana mapepo yalikuwa yakiunguzwa moto wa Yesu Kristo. Hakika watu wa Morogoro sasa wanajivunia ohuyu Bwana Yesu kwa hale hyaliyotokea jana na yatakayoendelea kutokea kwa kipindi kizima ambacho watumishi hawa wa Mungu watakuwa wanafanya kazi ya Mungu

Mtume Peter Nyaga

Mtume Peter Nyaga wa kanisa la RGC Tabata Chang'ombe Dar es Salaama ameacha kanisa lake kwa lengo la kuja kuwasaidia hawa watu wa Morogoro walioteseka kwa muda mrefu kwa magonjwa na taabu mbalimbali, wametumikishwa na shetani vya kutosha. Wewe uliye Morogoro na mikoa ya jirani fika katika eneo la tukio upokea muujiza wako.


 







Tangazo limetengezwa na Rumafrica +255 851523
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...