MTUME NYAGA HR

AGALIA EMMANUEL TV LIVE [WATCH EMMANUEL TV LIVE]

Jumanne, 13 Mei 2014

NABII DR. LUCY NATASHA KUTOKA KENYA KUSHUSHA WINGU LA BARAKA KATIKA KONGAMANO LA AKINA MAMA NA MABINTI KATIKA KANISA LA RGC TABATA CHANG'OMBE - DSM TANZANIA

Watanzania umefika wakati wa kubanan kwa Yesu Kristo katika kanisa la RGC Tabata Chang'ome kwa Mtume anayetikisa hapa mjini Mtume Peter Nyaga. Mungu ameamua kuongea na akina mama na mabinti katika kongamano litakaloongozwa na watumishi wa Mungu wapatao nane wakivamia madhabahu moja huku wakitumia MIC moja siku hiyo.

Kilichonifurahisha ni pale Nabii mrembo aliyeumbika vizuri kwa kazi ya Mungu kutoka Kenya Nabii Dr. Lucy Natasha ambaye amehubiri sehemu nyingi sana duniani. Nabii huyu amepewa kazi na Mungu ya kuwaleta kuwakomboa waliopotea na kuhakikisha waliokombolewa wanaziidi kufurahi ukombozi wao mpaka siku ile ya mwisho. Jukumu lake ni kuhakikisha anafanya kila awezalo kumtukuza Mungu wetu na kutagaza habari njema za Mungu.


Nabii Dr. Lucy Natasha (Kenya)

Usikose kabisa mwana wa Mungu katika kongamano hili lenye waimbaji zaidi ya kumi kuvamii madhabahu moja kwaajili yako wewe UBARIKIWE. Mtaarifu na jamaa yako ili siku hiyo ashuhudie ishara na miujiza ya BWANA..

Mtume Peter Nyaga na mke wa Mchungaji Anna Nyaga wamejipanga kabisa kuhakikisha huu ugeni utakaofika katika kanisa lake utakuwa salama. Na eneo la kanisa lake kuzungukwa na nguvu za Mungu zitakazokuhamisha wewe katika mazingira uliyozoea na kuingia katika mazingira mengine tofauti.

Waimbaji kama Sarah Mvungi, Madam Ruti, Masanja Mkandamizaji, Mess Jacob Chengula, Martha Mwaipaja, Neema Gasper na wengine wengi watahakikisha kazi ya BWANA wetu YESU KRISTO inajidhihirisha kwako wewe utakayefika siku hiyo.


Tangazo limetengezwa na Rumafrica +255 715 851523

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...