MTUME NYAGA HR

AGALIA EMMANUEL TV LIVE [WATCH EMMANUEL TV LIVE]

Alhamisi, 4 Julai 2013

LIVE:MKUTANO WA KUOMBEA AMANI NA MITUME SABA KATIKA MADHABAHU MOJA RGC TABATA CHANG'OMBE

Siku ya leo matendo makuu ya Mungu yafanyika katika knisa la RGC Miracle Center kwa Mtume Peter Nyaga. Na leo kutakuwa na wahubiri mbalimbali watakaohubiri mahali hapa. Kuna Mtume Onesmo Ndegi wa kanisa la Makuti Kawe, Mtume Nyarusi, Nabii Joshua na Mtume Munene

Ninakukaribisha katika mkutano huu unaoendelea hapa kanisani kwa Mtume Peter Nyaga wa kanisa la RGC Tabata Chang'ombe. Watu ni wengi sana wanamiminika kuja kumtukuza Mungu.







GRACE MWAIPOPO





MARTIN MALUNGA KUTOKA KENYA




GRACE WA PRAISE TEAM RGC


 

 








PRAISE TEAM YA RGC TABATA CHANG'OMBE KUFUNGUA MKUTANO KWA MAOMBI
















MTUME PETER NYAGA AKIFUNGUA MKUTANO KWA MAOMBI NA
Ninawasalimu kwa jina la Yesu. Ninaitwa Mtume Nyaga nimeokoka na kusamehewa dhambi. Leo ni siku ya nne na Mungu anaenda kufanya kitu kipya juu ya maisha yako..

KUSUDI LA MUNGU KUUMBA MWANADAMU
kuna kusudi la Mungu kwako Mtanzania linalosababisha wewer uitwe Mtanzania na kuwepo duniani. Mwanzo 1:26 Mungu aliumba vitu vya kutawala na siku ya sita Mungu aliumba kila kitu. Kuumbwa kwako wewe kuna vitu Mungu ameumba wewe uweze kutawala, uwe umesoma au hujasoma. Kuna mbingu inatambua kuwa kuna vitu viko kwaajili yako au kwa mtu mwingine.

Kutokumiliki sio dhambi ya Mungu wala Mungu hana makosa, kabla hujaumbwa Mungu aliumba vitu vya kumiliki.Mungu akikusaidia kumiliki hiyo nguo yako basi unauwezo wa kumiliki vikubwa. Kongamano letu hili ni la kutawala na kumiliki. Kuna vitu vingine Mungu amekusudia kumiliki lakini kuna adui anazuia kumiliki, ila ukiwa na Mungu utamiliki.

Utamiliki baraka za mwilini na baraka za rohoni. Muombe Mungu akumilikishe ardhi na sio vitu vingine. Unajua kuwa sisi tuliumbwa kwa udongo na tutazikwa udongoni,, kwahiyo ardhi ni muhimu sana katika maisha yako.

kESHO TUTAJIFUNZA JUU YA  KUZUIA VITU VINAVYOSABABISHWA KUTOTAWALA





KITABU CHA NGUVU ZA FEDHA KUPATIKANA RGC TABATA CHANG'OMBE KWA BEI YA TSH 5000. NI KITABU KIPYA NA LEO KIMEZINDULIWA KATIKA KANISA HILI NA MTUME PETER NYAGA
 
 

 


MTUME MNENE KUTOKA KENYA
Atahubiri siku ya kesho juu ya ujasiriamali








MTUME ONESMO NDEGI
Atahubiri siku ya Jumamosi na leo yuko katika nyumba ya Bwana





 













Mtume Peter Nyaga


MTUME NYARUSI AKIHUBIRI SASA HIVI

TAFUTA KUSAIDIWA NA BWANA

Isaya 42:23
Mambo ya siri ni ya Mungu wetu na Mungu ana mambo yaliyofunguliwa. Kuna mambo ambayo Mungu alishayafungua. Baraka ambazo zitakufuata na kukupata jioni ya leo. Mungu anaongoza ulimwengu huu kwa principles. Ukizidiwa principle za Bwana miiujiza itakujia na sio wewe kuifuta.
Isaya 41:11-13


Mtume Nyarusi akihubiri siku ya leo

Zaburi 108:12 Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu. Wokovu wa mwanadamu haufai kitu. Msaada wa Mungu unaingilia kati ya mambo yako.

Mtumishi wa Mungu Mtume Nyarusi akihubiri Neno la Mungu siku ya leo

Ninasema huwezi kumiliki kama huna kitu, kwani mfalme anatawala pamoja na kanisa.Mungu wa mitume saba anawatumia ili mkamiliki na kutwala vitu vya duniani na mbinguni.


Kusudia jumla kuwa duni imetosha, kudharauliwa, kumwa, kulaaniwa, kuchawiwa, kuwa mkia, imetosha. Kusudia


Ingawa uduni umeonekana na wakukataliwa Mungu ndiye njia ya uduni wako na kukataliwa kwako.Kuna watu wanaenda kutoka katika umaskini na uduni kinyume na utaratibu.Bwana atakupa kufanya, pokea neema ya kushinda umaskini. Shinda umaskini ukiwa katika hali duni na utaenda kumiliki na kumilikishwa. Mwanzo 27:38-40


Kulia ni Nabii Joshu, Mtume Peter Nyaga na Mtume Onesmo Ndegi

Mwanzo 27:38-40. Hata kama ulitenda djhambi isiyofaa na mambo yako yakawa yameharibika, mimi ninasema neema inakufuta kwani umemrudia Mungu wako. Unaweza kugeza hali uliyokuwa nayo utakapoponyoka.
Ni haki yako kumiliki na kutawala sasa, na ninamuomba Mungu aingilie kati katika maisha yako na upoke.



NABII JOSHUA AKIHUBIRI SASA

Wakati Mtu akiamua kutoroka hajali mlango wala ukuta wa kutoka. Wakati majini wanatafuta pakutokea wewe utapata mlango wa kutokea. Jioni ya leo ni jioni ya ajabu maisha mwako, kuna operation ya ajabu leo. Lazaro alisema enough is enough, na mimi leo utaweza kutoroka.

Munguwetu sio mpiganaji bali ni mkufunzi kwasababu amejizungushia silaha za hatari. Amezungukwa na jshi kali sana. Paulo na Sila walipoimba

Mungu wetu ni mwanzo na mwisho na asiyevunjwavunjwa na chochote. Mungu wetu ni Mungu asiyevunjika kama vile wewe ulivyovunjikavunjika, kulogeka. Mungu wetu ni mwanzo na mwisho na upendo usio na mwisho, Mungu ni chanzo cha rehema unazozijua. Hakuna mwenye rehema zaidi ya Mungu. Ninakupa mfano wa mahakamani, mtu anaposhinda kesi wanasema huyu hakimu ni mzuri, na kama hukumpa hakimu pesa basi kesi yako itakuwa mbaya., Kuna watu wengi wakoi mahakamani bila ya hatia kwasababu hawana pesa za kuwaonga mahakimu. Mwanadamu hana pendo halisi. Mwanadamu unapata upendo unapompokea Mungu na kuokoka.

Mungu ni Munguy wa kusamehe amtakaye na haijalishi atokako wala mali zake au umaskini wake. Mungu wetu ni Mungu wa hasira, na Munguwetu ni Mungu wa kanuni. Mungu ana hasira na ghadhabu kuliko mtu yeyote akiamua kufanya anafanya bila ya mtu yeyote kumzuia. Munguwetu akiamua ameamua. Mungu akisimama katika hasira hamuogopio yeyote anafanya afanyacho.

Joshua 1:Mungu alimkasirikia Musa akamuinua Joshua. Manabii hawaogopi chochote, Nabii na Mitume hawaogopi kwasababu ni makamanda wa vita. Mitume hawaogopi, hawasukumiki,hawatishiki. Ninasema unavyohubiri injili usiogope wala usifuate watu wanasema nini. Simama kama Nabii au Mtume bila ya kuangalia nmaneno ya watu. Ukikuta mitume, jeshi la Mungu linamzunguka kumtetea.



 
 
 




NABII JOSHUA AKIWA KATIKA SIFA NA MWIMBAJI WA INJILI BAADA YA KUMALIZA KUHUBIRI





MAOMBI YA KUFUNGA MKUTANO WA KUOMBEA AMANI TANZANIA UKIFANYIKA MUDA HUU HAPA RGC TABATA CHANG'OMBE. NABII JOSHUA AKIONGOZA MAOMBI PAMOJA NA MITUME WALIOFIKA MAHALI HAPA











































Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...